

Nimepata habari muda huo kuwa Mheshimiwa Amina Chifupa amefariki dunia katika Hospitali ya Lugalo, Dar es Salaam. Nilipiga simu nyumbani kwa wazazi wangu Dar na kuambiwa kuwa walitangaza kwenye television na walikatisha kipindi cha Rebecca kusudi wa tangaze.
Mungu amlaze marehemu Amina mahili pema peponi. Amin.
Amina, ulikuwa shujaa kwa wanawake wengi, tutakukosa, Mola amekuchukua mapema mno. Ninalia pamoja na ndugu zako.
*******************************************************************
Comments za Baba mzazi wa marehemu kwenye Michuzi blog:
MH. AMINA CHIFUPA WA MPAKANJIA HATUKO NAYE TENA. KWA MUJIBU WA BABA YAKE MZAZI MZEE CHIFUPA (PICHANI) AMBAYE NIMEONGEA NAE DAKIKA TANO ZILOPITA, HAYATI AMINA AMEFARIKI SAA TATU KASOROBO USIKU HUU HOSPITALI YA JESHI YA LUGALO ALIKOKUWA AMELAZWA. MAKELELE YA VILIO YALITAWALA MAZUNGUMZO YETU KUTHIBITISHA HABARI HII YA KUSTUA.