
Kaburi la marehemu bibi yangu, Gandula Mary Makatochi. Alifariki 1977 nikiwa mwanafunzi wa Form One, Zanaki Girls Sec.

Manda saa za jioni, mnaona Ziwa Nyasa

Muhogo ni chakula kikuu huko Manda. Hivi sasa kuna ukame. Nashangaa kwenye picha naona kijani kijani, lakini nilivyokuwa huko kila kitu kilikuwa 'brown' shauri ya kukosa mvua! Ugali wa muhogo na dagaa wa Ziwa Nyasa tamu sana.

Nilionana na ndugu wengine sana huko Ilela. Wengi walinikumbuka kwa vile nilikuwa mtundu sana nuikiwa mdogo.

Kaburi la Marehemu baba mdogo, Prof. Crispin Hauli huko Ilela. Alipofariki mwaka 2001 alikuwa mbunge wa Ludewa na pia Naibu Waziri wa Fedha.

Njia kati ya Nsungu na Ilela, Manda Mnaona mlima wa Manda. Inaitwa Mt. Likolombola. (wadau naomba mnisaidie jina sahihi)

Ndugu huko Ilela Manda (Mama Nsumuka)

Niko na Ndugu wengine

Mimi na Bibi Mburuma, siyo bibi yangu lakini ni ndugu wa karibu.

Sara binti wa ndugu yangu Cassian ananisalimia

Niko na Happy, mtoto wa ndugu yangu Mama Rose