
Wadau, Ziwa Nyasa ni kubwa mno. Ni kama bahari. Ina mawimbi makali kama bahari. Nilitoka Dar es Salaam na basi, hadi Kyela. Nililala gesti (Pattaya Centre Hole) na asubuhi tuliondoka kuelekea bandarini. Kuna bandari mbili huko Kyela. Hii bandari tuliyoenda ni nje ya mji wa Kyela. Ukitaka kwenda Lupingu, Manda, Mbamba Bay na sehemu kadhaa unapanda meli hapo. Hiyo Meli inaendeshawa na Tanzania Railways.
Siku tuliyoondoka, Oktoba 29, 2009, ndo meli kubwa MV Songea ilikuwa inarudishwa katika huduma. Walikuwa wanaifanyia matengenezao ya mwisho mwisho. Walisema meli itaondoka saa 7 mchana, lakini iliondoka saa 11 jioni. Swahili Time kweli kweli. La sivyo ingebidi tupande meli ndogo MV Iringa kesho yake.
Muda wote huo wasafiri pale bandarini waliishia kuchomwa na jua kali. Yaani kali kuliko hata Dar es Salaam. Kulikuwa na akina mama na watoto wao wengi tu pale. Kivuli hakuna. Kulikuwa na vimiti, na pia kajumba. Hiyo jumba walisema inafunguliwa tu, kama kuna wasafiri wanaolala pale kungojea meli, mfano inachelewa kuondoka. Ofisi ya kuuza tiketi ni kontena.
Kundi la akina mama waliamua kwenda kupeleka watoto wao kuoga pale kwenye beach. Mimi mwenyewe nilitia miguu kwenye maji ili kupooza ile joto. Ajabu, polisi fulani mwenye cheo ndogo sana alitokea na kuwafukuza wale wakina mama na watoto wao pale kwenye maji. Halafu alikuwa anatukana matusi ya nguoni, ila watu wamsikie huko kavaa magwanda yake. Sijui alijiona mtu mkubwa sana kwa kitendo chake.
Ningeomba serikali waweke angalau kibanda chenye kivuli pale, bandari ili watu wasichomwe na jua.
Kuna akina Mama Ntilie pale, na wanapikaga dagaa safi sana!
Jua lina zama. Ziwa Nyasa imetulia.
Bado tuko Kyela
Siku tuliyoondoka, Oktoba 29, 2009, ndo meli kubwa MV Songea ilikuwa inarudishwa katika huduma. Walikuwa wanaifanyia matengenezao ya mwisho mwisho. Walisema meli itaondoka saa 7 mchana, lakini iliondoka saa 11 jioni. Swahili Time kweli kweli. La sivyo ingebidi tupande meli ndogo MV Iringa kesho yake.
Muda wote huo wasafiri pale bandarini waliishia kuchomwa na jua kali. Yaani kali kuliko hata Dar es Salaam. Kulikuwa na akina mama na watoto wao wengi tu pale. Kivuli hakuna. Kulikuwa na vimiti, na pia kajumba. Hiyo jumba walisema inafunguliwa tu, kama kuna wasafiri wanaolala pale kungojea meli, mfano inachelewa kuondoka. Ofisi ya kuuza tiketi ni kontena.
Kundi la akina mama waliamua kwenda kupeleka watoto wao kuoga pale kwenye beach. Mimi mwenyewe nilitia miguu kwenye maji ili kupooza ile joto. Ajabu, polisi fulani mwenye cheo ndogo sana alitokea na kuwafukuza wale wakina mama na watoto wao pale kwenye maji. Halafu alikuwa anatukana matusi ya nguoni, ila watu wamsikie huko kavaa magwanda yake. Sijui alijiona mtu mkubwa sana kwa kitendo chake.
Ningeomba serikali waweke angalau kibanda chenye kivuli pale, bandari ili watu wasichomwe na jua.
Kuna akina Mama Ntilie pale, na wanapikaga dagaa safi sana!

