
Kuna Dada fulani (jina ameomba nihifadhi) amenilietea maoni yake. Nazishea na wadau....
***********************************************************************
Dada Chemi ngoja leo nikudondoshee mtazamo wangu,mi nimpezi sana wa blog hii,na sababu kubwa iliyonifanya nipapende humu ni uandishi wako,na mimi nipe fulsa nikuandikie leo mtazamo wangu maana na mimi napenda saana kuandika.
Kitu ninachotaka kuwaeleza watanzania wenzangu,majirani au marafiki zetu hii leo ni kwamba tujijengee utamaduni wa kukubali kama tunaweza kufika kimaendeleo kama wenzetu waliotutangulia.
Mfano wangu nautoa humu humu kwenye pita yangu blogini mwako nikakuta picha mbalimbali za muigizaji maarufu wa Tanzania Steven Kanumba ,ambaye kajipatia umaarufu mkubwa katika sekta ya uigizaji hapa nchini akiwa ziarani Hollywood na uliandika Kanumba au kwa watu wanaomkubali humwita Denzel Washington wa bongo.
Sasa Dada Chemi ulileta mzozo pale ulivyosema Denzel Washington wa bongo,nilivyoona mimi nilifurahi na kusema “yes” siku moja Kanumba anaweza kufika hapo Denzel alipo lakini wasiwasi wangu ulikuwa kwenye maoni,nikasema sasa asubiri kushushuliwa na wabongo (maana ni kawaida yetu kutokukubali).
Nilifurahi sana kuona watu mbali mbali wakimpongeza na kukubali kazi yake,lakini kilichonisikitisha kuna wengi wadau hawakumkubali yeye afananishwe na denzel hata siku moja.Kwa kweli nilishwangazwa sana na kauli hizo.
Na huo ni mfano mmoja tu,kuna vitu vingi tu vinafanyika miongoni mwetu na uwa tunakatishana tamaa sana,wewe tu thubutu kumwambia mtu mipangilio yako ya baabae utaona ishu yake itakavyokuwa,”oh wewe utaweza kweli au walishafanya wakina fulani wakashindwa sembuse wewe” .
Sasa mi nilikuwa najiuliza wenzetu (Nchi nyingine) wakipiga hatua fulani ya juu,uwa wanawathamini na kuwaunga mkono kwa hatua waliyopiga,kwa nini na sisi tusibadilishe mioyo yetu na tujipende,kama mtu kafanya vibaya basi mshauri kama mtu kajitahidi kwenye maendeleo basi mpongeze,na kama ni mazuri yaige na wewe uwe na maendeleo kama hayo yake.
Kujikubali ni kukubali kwamba unaweza kufanya kitu chochote cha maendeleo ulichopanga na ukafanikiwa na hata zaidi yake,na hayo ndo maendeleo yenyewe,kama huo mfano wangu hapo juu wa Kanumba kuitwa Denzel Washington wa Bongo, sasa kwani Kanumba hawezi kuwa kama Denzel au zaidi?.
Nakumbuka mimi nilikuwa nataka kuanza biashara fulani hivi,nikamwaga aidia yangu kwa jamaa zangu fulani,unajua waliniambia nini,eti hiyo biashara ni ngumu sana na sitaweza kufika popote na nitapoteza muda na nguvu.
Kwa kweli niliumia na kuvunjika moyo kabisa,na mimi naye nikawaamini kwa kweli hata kasi ya kufanya hiyo biashara nikaacha kabisa,basi angalia yaliyofuata,baada ya mienzi kadhaa nikashangaa kuona hao hao walioniambia haiwezekani wakianzisha ishu iyo iyo niliyowapa kuomba ushauri kwao na hao hao ndo waliniambia haifai.
Kitu ninachotaka kusema hapa ,tujiamini kwa kila kitu tunachotaka kufanya,hakuna mtu anaweza kuondosha ndoto yako kwenye Dunia hii ila wewe mwenyewe, Kama mtu hakuamini basi wewe jiamini na unaweza.
Hivi unajua maendeleo mengine yanakuja pale wewe ukimuona mwenzio kafanya vizuri na wewe unataka kufanya kama yeye,lakini inaelekea wabongo wengi hatujui hilo na wanaoona ni wachache labda.
Zaidi ya yote tunatakiwa kukaza buti kisawasawa tusiruhu kukatishwa tamaa na wengine,tuamini kama kila mtu anauwezo na nafasi ya kufanya jambo la maendeleo bila kukatishwa tamaa,Lakini wabongo tubadilike tusiwasifie wenzetu tu na sisi tujikandamize kuwa ni dhaifu sana,au haujui mtu akisifia ndo bichwa linapanda na kufanya zaidi ili asikuangushe uliyemsifia(ha ha ni mawazo yangu tu).
Je unajua ni kwanini duniani wazungu wanajiona ni bora zaidi ya wengine?na wamejitangaza kwa kujisifia na kujikubali kwamba wao ni zaidi,na ngozi yao ni bora kuliko zingine?.Na hapo ndo maana kimaendeleo acha tu ya kiuchumi tunaiga kutoka kwao,na hata baadhi ya dada zetu wameamini hilo na kujibadilisha nao wawe weupee kama wazungu.
Mi siku nilijiuliza eti kama sisi weusi,tungekuwa wazungu na wazungu wangekuwa kama sisi,nywele rangi nk,Nafikiri tungelazimika kujibadili kama sasa tunavyotaka nywele ndefu laini nk.Hapo mi nafikiri wamefanya tuwaamini hivyo kwa sababu wanadhamini vito vyao zaidi na kuwaeleza wengine umuhimu wake hata kama si vizuri na vyakuigwa.