
Baada ya Disco 1979 shule ya wasichana ya sekondari Zanaki. Kati ni Mwalimu wetu wa Physics Mr. Tamba, wakati huo alikuwa anasoma Education University of Dar es Salaam ,Fourth year, na kaja kufanya Practicals.
Tuliomzunguka, mbele kabisa mimi, kulia kwangu ni Natujwa Mbagga ambaye siku hizi ni Mama Shilla. Patricia Kassamia, mwenye bun (nimesahau jina), Kulthum, na huyo dada mwingine alikuwa anasoma darasa la Commerce.

Mbele kuanzia kushoto - Mimi, Lilian Maganga, Emily Mbagule, Theresia
Nyuma kuanzia kushoto - Dorothy Kihampa, Neema Kingswaga, na (Jina nimesahau)

Hapa ni Darasa la Form Four Science One! Sayansi Wani! (Enzi hiyo top floor kwenye corner) na tulikuwa wanafunzi 25 tu kwenye hiyo darasa. Tulikuwa wasomi kweli, maana mwalimu alikuwa antoa tuition bure, lakini wachache walibakia kuifaidi. Karibu wote walioenda Form Five kutoka Zanaki mwaka huo walitoka darasa letu la Science One.
Mbele, kuanzia kushoto -Demetria Joseph, Lucy Masamba, Rosemary
Nyuma, kuanzia kushoto -Dorothy Kihampa, Batuli, na mimi
Historia fupi - Kabla ya kuwa Zanaki Girls, ilikuwa Aga Khan Girls School. Shule ilitaifishwa baada ya Azimio ya Arusha. Katika hiyo compound kulikuwa na shule ya vidudu (private) na shule ya msingi na Hostel. Nasikia Hostel imerudishwa kwa Aga Khan.
Sketi za bluu. Tulianza kuvaa sketi za bluu nikiwa Form Two. Kabla ya hapo walikuwa wanavaa sketi za kijani. Nakumbuka walifanya kama fashion show asubuhi wakati wa mazoezi na gwaride na hiyo design ya bluu ilichaguliwa.