Hivi majuzi kampa mke wake, Mheshimiwa Amina Chifupa, talaka na leo tunasikia yuko hoi kitandani! Mungu ampe nguvu maana mambo ya ndani yakianikwa hadharani yanaweza kuleta presha!

********************************************
From: http://www.ippmedia.com/ipp/alasiri/2007/05/09/90143.html
Mumewe Amina hoi!
2007-05-09 Na Badru Kimwaga, Jijini
Siku chache tu baada ya `kumlima` talaka mkewe kwa tuhuma za kutokuwa muaminifu, katika ndoa, mfanyabiashara maarufu nchini, Bwana Mohammed Mpakanjia almaarufu kama `Meddy` imedaiwa kuwa hivi sasa yuko hoi bin taaban kitandani.
Akizungumza na Alasiri kwa njia ya simu mapema leo asubuhi, mfanyabiashara huyo ambaye pia ni mkandarasi wa kutengeneza barabara, amesema hivi sasa yu hoi kitandani kutokana na kusumbuliwa na maradhi ambayo hakuweza kuyafichua.