

Kwa kweli mwaka huu nangojea kwa hamu siku ya May 28th. Siku hiyo NBC itonyesha Live mashindano ya Miss Universe itakayofanyika huko Mexico City.
Mwakilishi wa Tanzania, Flaviana Matata yumo. Kwa kweli weusi kutoka nchi zingine wana weave na wigi kichwani, lakini yeye kanyoa upara! Kama vile kusema, napenda uafrika wangu! Naomba afike mbali katika hayo mashindano.
Na hata kama hata pita msishangae mkisikia kuwa amepata modelling contract, au yuko kwenye matangazo ya magazeti na TV. Sasa hivi hao models weusi wa kiafrika ni mali kweli hapa. Washukuru akini Alek Wek, na Iman kwa kupendwa waafrika katika u-model hapa USA. Zamani ilikuwa model mweusi lazima awe mweupe karibia ya mzungu na awe na nywele ndefu!
Black Beauty juu! Waafrika tujipende!