
Wiki hii nilibahatika kumkabidhi aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania enzi za Rais Mkapa, Mheshimiwa Frederick Sumaye, DVD za sinema ya Tusamehe na Bongoland. Yeye ni jirani yangu hapa Cambridge, Massachusetts. Anasoma Harvard University.
Mheshimiwa Sumaye alifurahi sana kuona DVD hizo na alisema ingekuwa vizuri vijana wote Tanzania wazione kwani zina ujumbe nzito sana.
Katika sinema ya Tusamehe waTanzania waliofanikiwa kimaisha Marekani wanakumbwa na ugonjwa wa UKIMWI, na katika Bongoland, MTanzania anapambana na maisha Marekani.
Sinema hizo zimetengenezwa na mwanafilamu wa kiTanzania aishio huko Minnesota, Josiah Kibira. Kwa habari zaidi za sinema hizo na hata kununua DVD zake, tembelea....
http://www.kibirafilms.com/index.html