
Mgombea wa raisi wa Marekani katika uchaguzi ujao, Senator Barack Obama wa Illinois, amewekwa chini ya ulinzi ya Secret Service. Kazi ya Secret Service ni kulinda watu wazito katika serikali ya Marekani kama Raisi na familia yake na makamu wake, na pia wagombea raisi lakini walioteuliwa na vyama vyao.
Obama bado hajateuliwa, hivyo ina maana kuwa lazima Secret Service wamepata habari kuwa maisha yake iko hatarini. Kama tunavyojua Obama ni mweusi na bado kuna wabaguzi hapa Marekani amabao wasingependa kuona mtu mweusi anashika uraisi. Ametokea kupendwa na watu wa kila rangi na kuna watu ambao hawafurahii kabisa! Tusisahau viongozi weusi waliouliwa na hao wabaguzi kama Martin Luther King Jr., na Medgar Evers.
Mungu amlinde na abariki Barack Obama!
Mungu amlinde na abariki Barack Obama!
********************************************************************
Thursday, May 03, 2007
(CNN) Democratic presidential hopeful Barack Obama has been placed under secret service detail, according to a statement from the U.S. Secret Service."Secretary Chertoff has, after consultation with the congressional advisory committee, authorized the United States Secret Service, to protect presidential candidate Senate Barack Obama. "As a matter of procedure, we will not release any details of the deliberations or assessments that led to protection being initiated. For security reasons we will not release the timing, scope or details of any protective operations."