
DAH! Yaani wadau kwa kweli mnisamehe, maana hii habari ya Mhesimiwa Lowassa nimesikia saa hizi, 9:56Am (EST). Nilikuwa busy na mambo ya audition ya sinema fulani.
Kwa kweli nimeshutuka sana na nimesikitika mno hasa chanzo cha kujizulu kwake. Ila nimefurahi kuona kuwa Tanzania kuna haki ya kusema siku hizi, FREEDOM OF SPEECH. Na safari hii uchunguzi ulifanyika na haikutiwa maji!
Dr. Harrison Mwakyembe, NAKUSIFU! Bado unaujasiri wa enzi zile! Ila uko salama kweli sasa?
Haya tuone nani atateuliwa kuwa Waziri Mkuu sasa. Any suggestions/predictions?
*******************************************************************************
HABARI TOKA DODOMA SASA HIVI ZINASEMA KUWA SPIKA WA BUNGE MH. SAMWEL SITTA AMETANGAZA KWAMBA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA AMEAMUA KUJIUZULU UWAZIRI MKUU.
MH. SPIKA BAADA YA KUTANGAZA HILO AMESEMA MJADALA WA RIPOTI YA RICHMOND, NA SIO MJADALA WA LOWASSA, NDIO UENDELEE. NA NDICHO KINACHOFANYIKA HIVI SASA HUKO BUNGENI.
HABARI ZAIDI ZINASEMA KWAMBA MH. LOWASSA AMESEMA KWAMBA INGAWA HAJAMTAARIFU JK UAMUZI WAKE HUO, AMEAMUA KUJIWEKA KANDO!
*************************************************************
KARAMAGI NAYE AOMBA KUJIZULU!
KARAMAGI NAYE AOMBA KUACHIA NGAZI
MH. NAZIR KARAMAGI AMEMALIZA KUJIELEZA NA AMELIAMBIA BUNGE KWAMBA NA YEYE LEO ASUBUHI AMEPELEKA BARUA KWA JK KUOMBA KUJIUZURU WADHIFA WAKE WA UWAZIRI WA NISHATI NA MADINI.
YEYE PIA AMEJITETEA KWAMBA HANA HATIA KATIKA SAKATA HILI!
******************************************************************
MSABAHA NAYE AJIUZULU!
MSABAHA NAYE AMWAGA MANYANGA
WAZIRI WA AFRIKA MASHARIKI AMBAYE AWALI ALIKUWA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI DK MSABAHA NAYE KAMPELEKEA BARUA JK KUOMBA KUJIUZURU KWA MUJIBU WA MAELEZO YAKE ALIYOTOA DAKIKA HII BUNGENI
WHAT A SAD DAY IN TANZANIA POLITICS!