Wednesday, January 30, 2008

Mnenguaji Aisha Masinda anahitaji Msaada!

Wapendwa wadau,

Nimepokea hiii e-mail kuhusu Mnenguaji maarufu, Aisha Madinda, wa African Stars Band- Twanga Pepeta.

**********************************************************************

Habari yako, ukiwa kama mmmoja wa wazalendo naamini kabisa kwa namna moja ama nyingine utaguswa na ugonjwa unaomuandama Aisha MAdinda!

Aisha anahitaji msaada ili aweze kumudu matibabu anayoendelea nayo katika Hospital ya Taifa Muhimbili hivyo basi kama nawe utaguswa katika hili unaweza kwa kumsaidia kubandika habari hii niliyokutumia katika blog yako ili ujumbe huu uweze kusambaa zaidi!


Natanguliza shukurani zangu kwa kukubali kubandika habari hii!

Asante,
Tulizo Kilaga



****************************************************************************

Ugonjwa wa Aisha Madinda "Ngoma Nzito"


Ugonjwa wa Mnenguaji maarufu wa Bendi ya African Stars International, Aisha Madinda (27) hivi karibuni ulidhihilisha kuwa ni "ngoma nzito" kutokana na vipimo vya awali kuonesha asumbuliwi na ugonjwa wowote huku miguu ikiendelea kumvimba kila kukicha.

Aisha Madinda hivi karibuni alinukuliwa na gazeti moja la michezo nchini akisema kuwa, hali yake bado iko vile vile na miguu bado inamsumbua licha ya kufanyiwa uchunguzi wa awali.
Mnenguaji huyo aliongeza kuwa, kushindikana kuonekana ugonjwa wake kumesababisha madaktari bingwa wa moyo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam juzi (Jumatatu) mchana kuanza kumfanyia uchunguzi wa kina.

"Uchunguzi wa awali umeshindwa kubainisha ugonjwa wangu ndio wamenirudisha kwa madaktari bingwa wanifanyie uchunguzi zaidi, miguu imevimba na sijisikii vizuri, lakini kinachonisikitisha zaidi ni kutoonekana kwa maradhi yanayonisumbua. Nawaachia wataalam, nina imani kama kuna kitu hawa hawawezi kushindwa na suluhu ya tatizo langu itapatikana mapema, Mungu ni wa wote na naamini kwamba atanisaidia na hii ni hali ya kawaida tu kwenye maisha, wala siamini maneno ya watu kuwa nimepigwa juju," alisema Aisha.

Aisha Madinda ambaye ni mama wa watoto wawili wanaosoma sekondari, amekuwa nje ya jukwaa kwa zaidi ya miezi mitatu sasa kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa.

Mnenguaji huyo, amewaomba wadau mbalimbali na mashabiki wa muziki nchini kuendelea kumsaidia kwa hali na mali ikiwa ni pamoja na kugharamia matibabu yake kupitia namba 0717 555557 ambayo ni ya meneja wake.


Kutoa ni moyo si utajili mimi nimeanza kwa kumchangia kwa kuusambaza ujumbe huu!!
 

FREE HOT VIDEO 1 | HOT GIRL GALERRY 1

FREE HOT VIDEO 2 | HOT GIRL GALERRY 2

FREE HOT VIDEO 3 | HOT GIRL GALERRY 3

FREE HOT VIDEO 4 | HOT GIRL GALERRY 4

FREE HOT VIDEO 5 | HOT GIRL GALERRY 5

FREE HOT VIDEO 6 | HOT GIRL GALERRY 6

FREE HOT VIDEO 7 | HOT GIRL GALERRY 7

FREE HOT VIDEO 8 | HOT GIRL GALERRY 8

FREE HOT VIDEO 9 | HOT GIRL GALERRY 9

FREE HOT VIDEO 10 | HOT GIRL GALERRY 10

FREE HOT VIDEO 11 | HOT GIRL GALERRY 11