
Kuna habari kuwa Rais Bush ameibiwa saa yake ya mkononi akiwa kwenye ziara Albania. Wanasema kuwa Bush alifurahi sana jinsi wananchi wa walivyokuwa wanamshabikia kiasi kuwa aliamua kwenda kuwasalimia. Hiyo kusalimiana na wananchi haikupangwa. Ndo hapo wajanja wakawai saa yake.
Wengine wanasema hata pete yake ya ndoa ilibiwa pia.
Wanasema saa ilikuwa ya bei mbaya kweli. Lakini bila shaka ilikuwa na inusrance kali kama Lloyds of London.
Wanasema saa ilikuwa ya bei mbaya kweli. Lakini bila shaka ilikuwa na inusrance kali kama Lloyds of London.
Serikali ya Marekani inakataa kuwa saa yake iliibiwa. Lakini mbona video haidanganyi? Mara unaona saa mara haipo. Cha kuchekesha msemaji wake, Tony Snow, kasema "Baada ya kutazama video tulithibitisha kuwa saa yake haikuibiwa." Jamani! Kama haikuibiwa kwa nini mlitazama video kuona kama imebiwa?
Kwa habari zaidi someni: