

Miaka mingi nimeudhika sana na tabia ya wanaume kukataa watoto wao. Wanatembea na mwanamke, anapata mimba, na wanasema si wakwao. Mwanamke anabisha, na wanasema oh huyo mwanamke malaya katembea na wengine, huyo mtoto si wa kwangu. Nasema Shenzi Taipu mkome tabia yenu mbaya!
Halafu ndugu wanasema oh, sijui tungojeee tuone mtoto anafanana na nani. Loh, je kama mtoto anafanana na mwanamke na ndugu zake ndo mmepata kisingizio. Eh he! Si nilikuambia huyo mtoto si wakwangu. Pumbavu kabisa nyie wanaume, cheki dental formula ya mtoto mbona ina fanana na yako. Au mtoto kazaliwa na vidole sita kwenye mguu kama wewe, japo sura kafanana na mama yake. Wanaume kwa kupenda kukwepa majukumu yao!
Miaka mingi wazungu wamekuwa na njia za kugundua baba mtoto hasa ni nani. Walikuwa wanapima damu. Lakini siku hizi kuna 'fail proof' njia ya kuhakisha nayo ni DNA Testing. Na kama ulikuwa hutaki kupima utapimwa tu, maana kajinywele kinatosha kupima. Kama uliacha shahawa kwenye shuka inatosha kupimwa hata kama imekauka. Kama ulikuwa unapiga busu na mama mtu na kuacha denda kwenye blausi yake, inatosha kabisa kupata hiyo DNA. Hata kama umegusa mahala unaweza kuacha chembe chembe za ngozi na kupimwa DNA!
Kesi maarufu za DNA ni:
Mtoto wa marehemu Anna Nicole Smith. Wanaume wanne waligombania mtoto wake wa kike, DannieLynn na kudai ni wakwao kwa vile alitembea nao. Huyo mtoto ni bilionea maana anarithi mapesa ya mama yake. Basi, Anna kaolewa na mwanasheria wake, Howard Stern, huko wanaume wengine wanadai oh, mtoto wa kwao. Wote walipimwa DNA. Kumbe baba mtoto ni wa mpiga picha, Larry Birkhead. Duh! Baada ya testi huyo stern alimkabidhi mtoto kwa Birkhead bila ubishi wowote.
Na kwa sasa mcheza sinema Eddie Murphy anapimwa kwa ajaili ya mtoto aliyezaa Spice Girl Melanie Brown. Murphy anaseme mtoto wa Scary Spice si wa kwake, lakini mmh sijui kwa kumtazama tu naweza kusema hakuna haja hata ya kupima mtoto ni wa Murphy. Anywy, hiyo DNA test ndo itamaliza maswali yote.
Prince Harry, mtoto wa marehemu Princess Diana na Prince Charles (?) wa Uingereza. Watu wanadai ni mtoto wa mpambe wa Diana, James Hewitt, maana katembea naye akiwa ameolewa na Prince Charles. Harry mwenyewe anataka DNA test kujua nani baba yake amalize maswali ambayo yamemsumbua miaka mingi.
Halafu ndugu wanasema oh, sijui tungojeee tuone mtoto anafanana na nani. Loh, je kama mtoto anafanana na mwanamke na ndugu zake ndo mmepata kisingizio. Eh he! Si nilikuambia huyo mtoto si wakwangu. Pumbavu kabisa nyie wanaume, cheki dental formula ya mtoto mbona ina fanana na yako. Au mtoto kazaliwa na vidole sita kwenye mguu kama wewe, japo sura kafanana na mama yake. Wanaume kwa kupenda kukwepa majukumu yao!
Miaka mingi wazungu wamekuwa na njia za kugundua baba mtoto hasa ni nani. Walikuwa wanapima damu. Lakini siku hizi kuna 'fail proof' njia ya kuhakisha nayo ni DNA Testing. Na kama ulikuwa hutaki kupima utapimwa tu, maana kajinywele kinatosha kupima. Kama uliacha shahawa kwenye shuka inatosha kupimwa hata kama imekauka. Kama ulikuwa unapiga busu na mama mtu na kuacha denda kwenye blausi yake, inatosha kabisa kupata hiyo DNA. Hata kama umegusa mahala unaweza kuacha chembe chembe za ngozi na kupimwa DNA!
Kesi maarufu za DNA ni:
Mtoto wa marehemu Anna Nicole Smith. Wanaume wanne waligombania mtoto wake wa kike, DannieLynn na kudai ni wakwao kwa vile alitembea nao. Huyo mtoto ni bilionea maana anarithi mapesa ya mama yake. Basi, Anna kaolewa na mwanasheria wake, Howard Stern, huko wanaume wengine wanadai oh, mtoto wa kwao. Wote walipimwa DNA. Kumbe baba mtoto ni wa mpiga picha, Larry Birkhead. Duh! Baada ya testi huyo stern alimkabidhi mtoto kwa Birkhead bila ubishi wowote.
Na kwa sasa mcheza sinema Eddie Murphy anapimwa kwa ajaili ya mtoto aliyezaa Spice Girl Melanie Brown. Murphy anaseme mtoto wa Scary Spice si wa kwake, lakini mmh sijui kwa kumtazama tu naweza kusema hakuna haja hata ya kupima mtoto ni wa Murphy. Anywy, hiyo DNA test ndo itamaliza maswali yote.
Prince Harry, mtoto wa marehemu Princess Diana na Prince Charles (?) wa Uingereza. Watu wanadai ni mtoto wa mpambe wa Diana, James Hewitt, maana katembea naye akiwa ameolewa na Prince Charles. Harry mwenyewe anataka DNA test kujua nani baba yake amalize maswali ambayo yamemsumbua miaka mingi.