

Photos from Michuzi Blog & Maggid Mjengwa Blog
Natoa pole, tena pole sana kwa Dada Amina Chifupa (Mbunge Viti Maalum). Miaka mingi nimekuwa nikifuatilia habari zake. Lakini hii miaka ya ya karibuni maisha yake yameanikwa hadharani na kushabikiwa kama vile maisha ya hao stars wa Hollywood. Yaani maisha yake imekuwa kama Tanzanian Soap Opera. Ni kama vile papparazzi wanavyofuatilia maisha ya Paris Hilton hapa Marekani..oh sijui kavaa hivi, katembea na huyo, alionekana sijui wapi! Khaa! Na inaelekea watu hawatosheki na habari wanazaopata kuhusu Dada Amina, wanataka zaidi na zaidi.
Kwa kweli tangu jana nilisikitika sana nilivyosikia kuwa mume wake kampa TALAKA! Nilidhania wana ndoa safi sana. Lakini tena ndoa yao naona imekuwa kama hizi ndoa za Hollywood, hazidumu!
Nampongeza Baba yake Luteni Chifupa kwa kuzuia Amina kufanya Press Conference kuhusu yaliompata. Ni mapema mno. Ngojea apoe kidogo maana lazima atakuwa ameshutuka mno, anaweza kuwa na hasira na kusema maneno ya ajabu na baadaye kujuta.
Sijui kama habari nilizosikia juu ya kisa cha Dada Amina kuachika ni kweli. Lakini kama ni ya kweli basi ni aibu kwa huyo mwanaume. Je, alishindwa kumtosheleza mke wake kwenye mambo ya unyumba? Hatimaye ukweli utajulikana.
Dada Amina, kumbuka kuwa watu watasema na mwisho watachoka! Nyayua kichwa juu ukitembea barabarani wala usijali maneno ya watu. Unajua maisha yako mwenyewe. Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu. Pia wanaume wako wengi katika dunia hii, na dunia ya leo si lazima uwe na mwanaume. Wakati mwingine mwanaume ni mzigo na mzuia maendeleo ya mwanamke. Samahani nimeingiza 'women's lib' hapa!
Na ambaye anatarajia kuolewa na huyo Bwana Mpakanija ajue kuwa atamtendea kama alivyomtendea Dada Amina. Kwa bahati mbaya ndivyo wanaume walivyo...wakimtendea mwanamke moja hivi na mwingine atatendewa vile vile.
Pamoja na kuwa nimemsema Bwana Mpakanija natoa pole kwake maana ni hatua kubwa aliyochukua na maisha yake pia yameanikwa hadharani. Jamani, mbona mlivyofunga ndoa mlionekana mna mapenzi mno.
Karibuni mtoe maoni.
Kwa habari zaidi ya Mheshimiwa Dada Amina Chifupa someni: