

Poleni waKorea wote. Sasa asante Cho Seung-Hui, itakuwa vigumu wapate visa za kuja kusoma Marekani bila kuchambuliwa kila kitu toka walichofanya toka wazaliwe mpaka wanakunya saa ngapi.
WaMarekani waoga sana na wabaguzi sana na sasa wamepata kisingizio cha kunyanyasa waKorea wote Marekani. Msisahau kabla ya 9/11 jinsi waarabu walivyokuwa wanathaminiwa Marekani shauri ya pesa zao.
Kama hamjasikia, vituko na visa vya kijana, Cho Seung-Hui, mwenye miaka 23, na mwanafunzi aliyekuwa anasoma Chuo Kikuu cha Virginia Tech nitawasimulia kwa ufupi. Siku ya jumatatu akili zilimruka na aliua wanafunzi na walimu wa chuoni hapo. Watu 32, walioamka na kufanya shughuli zao kama kawaida siku hiyo walipoteza maisha yao.
Cha ajabu, watu walijua kuwa huyo jamaa ni mwendawazimu siku nyingi. Hata mwalimu wake alienda polisi kumshitaki kuwa ana wasiwasi naye. Lakini polisi hawakufanya kitu.
Na wote tunajua mweusi angekuwa na vituko kama vyake, angefukuzwa shule zamani. Cho alikuwa anadika michezo ya kuigiza na mashairi zenye plots za kutisha kama kubaka, kuua, na kujiua.
Nani asiyejue kuwa waMarekani wanasema kuwa hao wenye asili ya Asia wana akili sana. Na si ajabu ndo maana huyo Bwana John Markell, alimwuzia bastola bila maswali mengi. Alisema, “he looked like a clean cut College student”, yaani alionekana hana matatizo. Je, kijana mweusi anayesoma Chuo Kikuu angeweza kununua bastola kwenye duka lake kwa urahisi hivyo? Na leo asubuhi nilikuwa nabishana na bosi wangu kuhusu hiyo swala, nikamwambia, huyo Markell asingeniuzia mimi mwanamke mweusi hiyo bastola, lazima angetafuta kisingizio cha kutokuniuzia maana sionekani kama clean cut college student au clean cut period.
Kati ya hao waliouliwa siku ya jumatatu kulikuwa na weusi kadhaa. Mmoja ni Ryan Clark, aliyekuwa na akili sana na kusoma Major tatu (haya nyie wazungu mnaosema kuwa weusi hawana akili). http://www.wrdw.com/news/headlines/7071667.html
Na jambo lingine kinachoniudhi. Wansema kuwa haya ndo mauaji makuu yaliyowahi kutokea nchini Marekani. Wamekosea, au wansema hivyo kwa vile weusi siyo watu kwao. Miaka ya nyuma huko Florida (1923) walikuwa mamia ya weusi, na mauaji ya weusi yalitokea Arkansas (1919) na Oklahoma (1921) pia.
Karibuni mtoe maoni yenu.
WaMarekani waoga sana na wabaguzi sana na sasa wamepata kisingizio cha kunyanyasa waKorea wote Marekani. Msisahau kabla ya 9/11 jinsi waarabu walivyokuwa wanathaminiwa Marekani shauri ya pesa zao.
Kama hamjasikia, vituko na visa vya kijana, Cho Seung-Hui, mwenye miaka 23, na mwanafunzi aliyekuwa anasoma Chuo Kikuu cha Virginia Tech nitawasimulia kwa ufupi. Siku ya jumatatu akili zilimruka na aliua wanafunzi na walimu wa chuoni hapo. Watu 32, walioamka na kufanya shughuli zao kama kawaida siku hiyo walipoteza maisha yao.
Cha ajabu, watu walijua kuwa huyo jamaa ni mwendawazimu siku nyingi. Hata mwalimu wake alienda polisi kumshitaki kuwa ana wasiwasi naye. Lakini polisi hawakufanya kitu.
Na wote tunajua mweusi angekuwa na vituko kama vyake, angefukuzwa shule zamani. Cho alikuwa anadika michezo ya kuigiza na mashairi zenye plots za kutisha kama kubaka, kuua, na kujiua.
Nani asiyejue kuwa waMarekani wanasema kuwa hao wenye asili ya Asia wana akili sana. Na si ajabu ndo maana huyo Bwana John Markell, alimwuzia bastola bila maswali mengi. Alisema, “he looked like a clean cut College student”, yaani alionekana hana matatizo. Je, kijana mweusi anayesoma Chuo Kikuu angeweza kununua bastola kwenye duka lake kwa urahisi hivyo? Na leo asubuhi nilikuwa nabishana na bosi wangu kuhusu hiyo swala, nikamwambia, huyo Markell asingeniuzia mimi mwanamke mweusi hiyo bastola, lazima angetafuta kisingizio cha kutokuniuzia maana sionekani kama clean cut college student au clean cut period.
Kati ya hao waliouliwa siku ya jumatatu kulikuwa na weusi kadhaa. Mmoja ni Ryan Clark, aliyekuwa na akili sana na kusoma Major tatu (haya nyie wazungu mnaosema kuwa weusi hawana akili). http://www.wrdw.com/news/headlines/7071667.html
Na jambo lingine kinachoniudhi. Wansema kuwa haya ndo mauaji makuu yaliyowahi kutokea nchini Marekani. Wamekosea, au wansema hivyo kwa vile weusi siyo watu kwao. Miaka ya nyuma huko Florida (1923) walikuwa mamia ya weusi, na mauaji ya weusi yalitokea Arkansas (1919) na Oklahoma (1921) pia.
Karibuni mtoe maoni yenu.