
Hata Boston, tunakunywa Konyagi! Ni pombe ya aina ya pekee duniani na waTanzania tunaweza kujivunia kuwa na sisi tuna kikali chetu! Inatengenezwa na Tanzania Distillers.
Jana niliamua kustarehe kidogo na kikali. Huwa napenda wine, au bia baridi! Lakini jana nilipata hamu ya Konyagi! Nilivyoenda Bongo mwaka jana nilirudi na kachupa ya Konyagi. Siku moja moja nikitaka kukumbuka 'home' nakunyawaga. Konyagi ni pombe enye ladha ya pekee. Halafu ni clear kuliko hata maji ya kunywa ya hapa Marekani.
Nashangaa haijanywa kinywaji kikuu ng'ambo kama vodka, najua unaweza kununua Uingereza lakini bado sijauona kwenye maduka ya pombe hapa USA. (Wasomaji mnishahishe kama nimekosea) Je, watengenzaji wamefanya international marketing?
Konyagi inatengenezwa na mabibo. Mnakumbuka tulivyokuwa tunaharibu nguo zetu na juisi ya mabibo. Doh! Pale UDSM, kati ya Hall 3 na Hall 2, kuna orchard kubwa kweli ya mikorosho. Tulikuwa tunashinda huko tuna chuma maikorosho, una kula ile bibo enye juisi kibao na korosho unatupa kwenye mfuko. Mfuko ukijaa unachukua kipande cha bati, halafu unatengeneza moto juu! Tia hizo korosho, na kaa mbali maana moshi huo! Nyie korosho zile za kuchuma na kuchoma wenyewe ni tamu.
Basi niwape story. Mara yangu ya kwanza kunywa Konyagi nilikuwa JKT. CO (Commanding Officer) alikuja Officer's Mess na kunipa offa. Nilmshukuru lakini ilibidi nikatae maana nilikuwa sijaozea kunywa pombe.
OHOOO! Si jamaa kanipa amri sijui adhabu ninywe nusu glass straight mbele yake! Niliinywa kama sumu, baada ya hapo nikaenda bweneni kulala hadi asubuhi huko tumbo na kichwa kinaumwa!
Lakini Konyagi kwa kiasi si mbaya hasa ukichanganywa na soda. Msinywe sana maana inalewesha haraka!
Konyagi JUU!